KLINIKI YA MADAKTARI BINGWA WA MAGONJWA YA NDANI, MIFUPA NA MFUMO WA MKOJO

TANGAZO LA HUDUMA ZA KIBINGWA
Uongozi wa Hospitali ya Songambele iliyopo katika kijiji cha Nkololo- Bariadi, unapenda kuwatangazia wakazi wote kuwa kutakuwa na ujio wa Madaktari Bingwa. Kutakuwa na Daktari Bingwa wa Mifupa, Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Ndani (Physician) na Daktari Bingwa wa Ngozi kuanzia tarehe 23/02/2026 hadi tarehe 27/02/2026.
Huduma zitakazotolewa kwenye klinic ya Magonjwa ya Mifupa:-
Matatizo ya Maumivu Makali ya Mgongo, Nyonga na Mifupa, Miguu kuwaka Moto, Ganzi, jointi za Mifupa, Matatizo ya mivunjiko mbalimbali iliyounga vibaya au iliyoshindikana kuunga, na Miguu iliyopinda (Matege).
Huduma zitakazotolewa na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Ndani ni:-
Magonjwa ya kisukari, Shinikizo la Damu (Presha), Magonjwa ya Moyo, Kiharusi (Stroke), Kifua kuuma au kubana (Pumu), Magonjwa ya Figo, Vidonda vya Tumbo, Pamoja na mengine mengi.
Huduma zitakazotolewa na Daktari Bingwa wa Mfumo wa Mkojo.
Wenye matatizo ya mfumo wa mkojo yaani U.T.I sugu, kukojoa kwa shida au kushindwa kukojoa, matatizo ya figo, tezi dume, maumivu wakati wa kukojoa, kupungua nguvu za kiume, kutoa usaha wakati wa kukojoa, maumivu ya tumbo la chini pamoja na mengine mengi
Pia huduma za Daktari bingwa wa magonjwa ya koo,pua, masikio, yanatolewa kila wiki siku ya Alhamisi.
Huduma za kila siku za Meno zinatolewa yaani Kutoa jino, Kuziba Jino, Kusafisha kinywa, Kupanga meno na kutibu harufu Mbaya Mdomoni.
HUDUMA ZITATOLEWA KWA MALIPO YA PAPO KWA PAPO, PAMOJA NA BIMA ZA NHIF NA BRITAM.
MAWASILIANO 0686-031556

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *